عربيEnglish

مريم ابنت عمران عليها السلام موسوعة القرآن الكريم

Towards providing reliable exegeses and translations of the meanings of the Noble Qur'an in the world languages

Those who set the ranks [As-Saaffat] - Swahili translation - Ali Muhsen Al-Berwani

Surah Those who set the ranks [As-Saaffat] Ayah 182 Location Maccah Number 37

Naapa kwa wanao jipanga kwa safu. [1]

Na kwa wenye kusoma Ukumbusho. [3]

Hakika Mungu wenu bila ya shaka ni Mmoja. [4]

Isipo kuwa anaye nyakua kitu kidogo, na mara humfwatia kimondo kinacho ng'ara. [10]

Bali unastaajabu, na wao wanafanya maskhara. [12]

Na husema: Haya si chochote ila ni uchawi tu ulio dhaahiri. [15]

Watasema (wakubwa): Bali nyinyi wenyewe hamkuwa Waumini. [29]

Basi hukumu ya Mola wetu Mlezi imekwisha tuthibitikia. Hakika bila ya shaka tutaonja tu adhabu. [31]

Tulikupotezeni kwa sababu sisi wenyewe tulikuwa wapotovu. [32]

Basi wao kwa hakika siku hiyo watashirikiana katika adhabu pamoja. [33]

Na wakisema: Hivyo sisi tuiache miungu yetu kwa ajili ya huyu mtunga mashairi mwendawazimu? [36]

Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio khitariwa. [40]

Wanazungushiwa kikombe chenye kinywaji cha chemchem. [45]

Na watakuwa nao wanawake wenye macho ya staha mazuri. [48]

Hao wanawake kama mayai yaliyo hifadhika. [49]

Aseme msemaji mmoja miongoni mwao: Hakika mimi nalikuwa na rafiki. [51]

Aliye kuwa akinambia: Hivyo wewe ni katika wanao sadiki. [52]

Na lau kuwa si neema ya Mola wangu Mlezi bila ya shaka ningeli kuwa miongoni mwa walio hudhurishwa. [57]

Hakika Sisi tumeufanya huo kuwa ni mateso kwa walio dhulumu. [63]

Mashada ya matunda yake kama kwamba vichwa vya mashet'ani. [65]

Kisha juu yake wanyweshwe mchanganyo wa maji yamoto yaliyo chemka. [67]

Kisha hakika marejeo yao bila ya shaka yatakuwa kwenye Jahannamu. [68]

Isipokuwa waja wa Mwenyezi Mungu waliokhitariwa. [74]

Na tukamwachia (sifa njema) kwa walio kuja baadaye. [78]

Kwa hakika hivi ndivyo tunavyo walipa wanao fanya mema. [80]

Kwa kuzua tu mnataka miungu mingine badala ya Mwenyezi Mungu? [86]

Mnamdhania nini Mola Mlezi wa walimwengu wote? [87]

Akasema: Hakika mimi ni mgonjwa! [89]

Akasema: Hivyo mnaviabudu vitu mnavyo vichonga wenyewe [95]

Na hali Mwenyezi Mungu ndiye aliye kuumbeni nyinyi na hivyo mnavyo vifanya! [96]

Na akasema: Hakika mimi nahama, nakwenda kwa Mola wangu Mlezi; Yeye ataniongoa. [99]

Ewe Mola wangu Mlezi! Nitunukie aliye miongoni mwa watenda mema. [100]

Basi wote wawili walipo jisalimisha, na akamlaza juu ya kipaji. [103]

Basi tukamtolea fidia kwa dhabihu mtukufu. [107]

Na tukamwachia (sifa njema) kwa watu walio kuja baadaye. [108]

Hivi ndivyo tunavyo walipa wanao fanya mema. [110]

Na tukambashiria kuzaliwa Is-haqa, naye ni Nabii miongoni mwa watu wema. [112]

Na hakika Ilyas bila ya shaka alikuwa miongoni mwa Mitume. [123]

Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wenu na Mola Mlezi wa baba zenu wa zamani?. [126]

Wakamkadhibisha. Basi kwa hakika watahudhurishwa;. [127]

Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio safishwa. [128]

Na tumemwachia (sifa nzuri) kwa walio kuja baadaye. [129]

Na hakika Lut'i bila ya shaka ni miongoni mwa Mitume. [133]

Isipo kuwa mwanamke mkongwe katika wale walio bakia nyuma. [135]

Akaingia katika kupigiwa kura, na akawa katika walio shindwa. [141]

Samaki akammeza hali ya kuwa ni mwenye kulaumiwa. [142]

Na ingeli kuwa hakuwa katika wanao mtakasa Mwenyezi Mungu,. [143]

Basi waulize: Ati Mola wako Mlezi ndiye mwenye watoto wa kike, na wao wanao watoto wa kiume?. [149]

Mwenyezi Mungu amezaa! Ama hakika bila ya shaka hao ni waongo!. [152]

Subhana 'Llah Ametakasika Mwenyezi Mungu na hayo wanayo msingizia. [159]

Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio safishwa. [160]

Na hakika bila ya shaka sisi ndio wajipangao safu. [165]

Na hakika sisi ndio wenye kusabihi kutakasa. [166]

Na walikuwapo walio kuwa wakisema:. [167]

Bila ya shaka tungeli kuwa ni waja wa Mwenyezi Mungu wenye ikhlasi. [169]

Ya kuwa wao bila ya shaka ndio watakao nusuriwa. [172]

Subhana Rabbi'l'Izzat Ametakasika Mola Mlezi Mwenye enzi na yale wanayo mzulia. [180]

Na sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa walimwengu wote. [182]